HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 13, 2016

TAASISI YA BINTI FOUNDATION YAKUTANA NA WAZAZI WA WATOTO WANAOWASAIDIA

 Mwanamitindo, Kulthum Sadiq akizungumza na wazazi wa watoto wanaosaidiwa na Taasisi ya Binti Foundation katika Shule ya Msingi Kumbukumbu jijini Dar es Salaam. Kulia ni Msimamizi wa Miradi wa taasisi hiyo, Jackline Kaiza. (Picha na Francis Dande)
Baadhi ya wazazi.
Mwalimu wa taaluma wa Shule ya Msingi Kumbukumbu, Fundikira akizungumza na wazazi wa watoto wanaosoma katika shule ya msingi Kumbukumbu.

NA NEEMA MWAMPAMBA

JAMII imeaswa kuacha kuwatumikisha watoto katika biashra pindi wanapotoka shule nyakati za jioni na badala yake wawapatie muda wa kujifunza.

Wito huo ulitolewa jana jijini Dar es Salaamna mbunifu wa mavazi na Katibu wa Taasisi ya Binti Foundation Kulthum Sadiq wakati alipokutana na wazazi watoto wanaosaidiwa na taasisi hiyo kwenye shule ya msingi Kumbukumbu.

Mwanamitindo huyo alisema alikutana na watoto wanaowasaidia kujua mambao yanayowakwamisha kufanya vizuri ambapo wengi walilamikia kutumikishwa na wazazi wanapotoka shule.

Alisema ili mtoto afanye vizuri na kufikia kama walipo watu maarufu   ulimwenguni lazima apate elimu katika mazingira bora.

Pia Binti foundation inatarajia kutoa mikopo kwa wazazi wa watoto wanaowasaidia ili kuweza kufanya biashara mbalimbali zitakazowawezesha kupata fedha za kuwahudumia watoto hao wanapokuwa katika masomo.

"Tumeyasikiliza matatizo na tutayachukua kuyafanyia kazi ikiwa ni pamoja na kuwapatia fedha za kufanya biashara mbalimbali zitakazowapa kipato muache kuwatumikisha watoto"alisema Sadiq.

No comments:

Post a Comment

Pages